Walioitwa Kazini Kutoka Usaili wa Sekta ya Umma
Walioitwa Kazini Kutoka Usaili wa Sekta ya Umma

Walioitwa Kazini Kutoka Usaili wa Sekta ya Umma – Tarehe 17 Aprili, 2025

TANGAZO: Walioitwa Kazini Kutoka Usaili wa Sekta ya Umma – Tarehe 17 Aprili, 2025

Dodoma, 17 Aprili 2025 — Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imetoa tangazo rasmi la kuitwa kazini kwa waombaji kazi waliofaulu usaili uliofanyika kati ya tarehe 02 Septemba 2024 hadi 18 Februari 2025, pamoja na wale waliokuwa kwenye kanzidata (Database) waliopangiwa vituo vya kazi baada ya nafasi kuibuka.

Kwa mujibu wa tangazo hilo, waombaji wote waliofaulu wanapaswa kuchukua barua zao za kupangiwa kituo cha kazi ndani ya siku saba kuanzia tarehe ya tangazo (yaani kuanzia leo), katika ofisi za Sekretarieti ya Ajira zilizopo Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kwenye majengo ya Dkt. Asha-Rose Migiro. Baada ya muda huo, barua ambazo hazitachukuliwa zitatumwa kwa wahusika kupitia anuani zao za Posta.

Aidha, wahitimu wote wanatakiwa kuripoti kwa waajiri wao kwa muda uliobainishwa kwenye barua hizo, wakiwa na vyeti halisi vya masomo kwa ajili ya uhakiki kabla ya kupewa barua ya ajira rasmi. Kwa wale ambao majina yao hayapo kwenye tangazo hili, inathibitishwa kuwa hawakufanikiwa kupata nafasi kwa wakati huu — lakini wanahimizwa kuendelea kuomba nafasi pindi zitakapojitokeza.

MUHIMU:

Wanaokuja kuchukua barua wanapaswa kuwa na mojawapo ya vitambulisho vifuatavyo kwa ajili ya utambuzi:

  • Kitambulisho cha Uraia (NIDA)

  • Hati ya Kusafiria

  • Kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi

  • Kitambulisho cha Mpiga Kura

  • Leseni ya Udereva

Tangazo linajumuisha majina ya walioitwa kutoka halmashauri mbalimbali kama vile Wanging’ombe, Njombe, Tandahimba, Mbarali, Mbogwe, Pangani, Kishapu, Newala, pamoja na taasisi kama Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC). Kada zilizohusika ni pamoja na walimu wa masomo mbalimbali, maafisa afya, wauguzi, mafamasia, maafisa sheria, na wateknolojia wa maabara.

Kwa orodha kamili ya majina ya walioitwa kazini, tafadhali [bofya hapa kupakua PDF kamili] na uone kama jina lako limo kwenye orodha hiyo 👉  PDF

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa matangazo mengine ya Ajira- Whatsapp

Mapendekezo Mengine;

Comments

No comments yet. Why don’t you start the discussion?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *