TANGAZO: Walioitwa Kazini Kutoka Usaili wa Sekta ya Umma – Tarehe 17 Aprili, 2025
Dodoma, 17 Aprili 2025 — Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imetoa tangazo rasmi la kuitwa kazini kwa waombaji kazi waliofaulu usaili uliofanyika kati ya tarehe 02 Septemba 2024 hadi 18 Februari 2025, pamoja na wale waliokuwa kwenye kanzidata (Database) waliopangiwa vituo vya kazi baada ya nafasi kuibuka.
Kwa mujibu wa tangazo hilo, waombaji wote waliofaulu wanapaswa kuchukua barua zao za kupangiwa kituo cha kazi ndani ya siku saba kuanzia tarehe ya tangazo (yaani kuanzia leo), katika ofisi za Sekretarieti ya Ajira zilizopo Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kwenye majengo ya Dkt. Asha-Rose Migiro. Baada ya muda huo, barua ambazo hazitachukuliwa zitatumwa kwa wahusika kupitia anuani zao za Posta.
Aidha, wahitimu wote wanatakiwa kuripoti kwa waajiri wao kwa muda uliobainishwa kwenye barua hizo, wakiwa na vyeti halisi vya masomo kwa ajili ya uhakiki kabla ya kupewa barua ya ajira rasmi. Kwa wale ambao majina yao hayapo kwenye tangazo hili, inathibitishwa kuwa hawakufanikiwa kupata nafasi kwa wakati huu — lakini wanahimizwa kuendelea kuomba nafasi pindi zitakapojitokeza.
MUHIMU:
Wanaokuja kuchukua barua wanapaswa kuwa na mojawapo ya vitambulisho vifuatavyo kwa ajili ya utambuzi:
-
Kitambulisho cha Uraia (NIDA)
-
Hati ya Kusafiria
-
Kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi
-
Kitambulisho cha Mpiga Kura
-
Leseni ya Udereva
Tangazo linajumuisha majina ya walioitwa kutoka halmashauri mbalimbali kama vile Wanging’ombe, Njombe, Tandahimba, Mbarali, Mbogwe, Pangani, Kishapu, Newala, pamoja na taasisi kama Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC). Kada zilizohusika ni pamoja na walimu wa masomo mbalimbali, maafisa afya, wauguzi, mafamasia, maafisa sheria, na wateknolojia wa maabara.
Kwa orodha kamili ya majina ya walioitwa kazini, tafadhali [bofya hapa kupakua PDF kamili] na uone kama jina lako limo kwenye orodha hiyo 👉 PDF
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa matangazo mengine ya Ajira- Whatsapp
Mapendekezo Mengine;
- Jinsi ya Kujisajili TaESA (Shirika la Huduma za Ajira Tanzania)
- Jinsi ya Kujisajili kwenye Ajira Portal Tanzania
- Jinsi ya Kutuma Maombi ya Ajira katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
- Nafasi za Kazi Kupitia Ajira Portal, Serikalini na Utumishi wa Umma 2025
- Jinsi ya Kupata Kazi Mapema (kwa Watafuta Ajira)
- Majina ya walioitwa kazini Sekta ya Afya 2025 TAMISEMI
- Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano 2025/2026 TAMISEMI